LOVESTORY MOVIES🔞 WAKUBWA TU

Ingia Hapa

Thibitisha Umri Wako

Je wewe ni mpenzi wa simulizi?

Hii ni kwawadau wanaopenda kusoma simulizi bonyeza button hiyo juu kisha chagua aina ya simulizi..

KARIBU KWA HUDUMA KAMA | GRAPHICS DESIGNER | MOVIES NA SERIES FULL HD | HUDUMA ZA MTANDAONI | VIFAA VYA COMPUTER NA MATENGENEZO | VIFAA VYA SIMU NA MATENGENEZO | KUTENGENEZEWA WEBSITE/BLOGS | WASILIANA NASI KUPITIA LIVE CHATI HAPO CHINI AMA TUPIGIE SIMU YA OFISI 0262605123

KAA KARIBU NASI KWA KUJIUNGA KATIKA GROUP LETU LA WHATSAPP HAPO CHINI

KWA WATEJA WETU WA MBALI LIPIA HUDUMA HAPA NA THIBITISHA MALIPO YAKO NASI TUKUHUDUMIE KWA UAMINIFU MKUBWA
📱JIUNGE NA GROUP LETU LA WHATSAPP

TANGAZA HAPA 🎉CHEZA USHINDE ZAWADI💰

GUSA ACHIA TWENDE CHUMBANI BABA MKWE 🔞

GUSA ACHIA TWENDE  CHUMBANI BABA MKWE
1....05
Sehemu ya kwanza.🔞

Wewe Muda wote niliokuacha bado unachambua matembele tu.

" Samahani mama mkwe nilikuwa nafagia kwanza.

" Koma sipendi kujibiwa mimi naongea na wewe unaongea.

" Nisamehe.

" Angalia mtoto wako umemlaza kwenye sofa apa ndio kitandani?

( Nikanyanyuka kumchukua mwanangu kwenye sofa bila kuongea)

" Wewe naongea peke yangu si ndio yani unanyanyuka kumchukua mtoto bila kujibu. 

( Nasikia sauti ya baba mkwe)

" Mke wangu una gubu sana mpaka umeniamsha mke wa mwanetu sijaona kosa lake ameanza kufagia kuweka mazingira sawa amekaa sasa kuchambua matembele umekuja na neno matembele kakujibu umemkomesha umelianzisha la mtoto ajakujibu unamswaga tena na maneno vaa kiatu icho chake wewe utajisikiaje?

" Mume wangu uyu mtoto ndio alale apa kwenye sofa akikojoa je?

" Mtoto wa miaka sita akojoe kweli kwenye sofa.

" Wewe unamjua uyu mtoto si amekuja nae tu kwenye ndoa.

" Mke wangu Leo kama umekasirishwa uko ulipotoka usije malizia hasira zako kwa mke wa mtoto wetu.

" Wewe mumeo akija niamshe na marufuku kulaza nyau wako apa kwenye sofa.

" Mama mkwe samahani mwanangu anaitwa halima aitwi nyau.

" Halima halima halima iyo halima kitumba au?

( Nilikaa kimya...mama mkwe akaingia ndani na baba mkwe akatulia sebuleni pale anaangaria mpira....nilikuwa nafanya  kazi uku nalia nakumbuka mengi Sana nilimwambia mume wangu unanioa si uhame kwenu akakataa na amenipenda mimi na mwanangu Leo namaliza   wiki mbili kwenye ndoa mama mkwe ameanza vituko...nikamaliza kuchambua matembele nikapika nikamaliza nilishindwa ata kula mala mume wangu analudi bahati nzuri mama yake alishaamka wanakutana sebuleni...mimi nipo chumbani nimejiinamia namsikia mama mkwe anasema)

" Juma ivi wanawake wasio na watoto uku waona?.

" Mama mbona sielewi swali lako?

" Uelewi nini wewe umekubali mpira uanze uku mwenzio ana goli moja huo si ujinga. 

" Sikuelewi bado mama.

" Nakuuliza uyu mtoto wa mkeo ukienda shule kumwandikisha utaandika JINA la nani?

" La baba yake.

" Ndio uwanaume huo unakaa unataja kabisa JINA la mwanaume mwenzio halima nyau paka kibichwa.

( Nilijikuta ndani chozi linanitoka kwanini mwanangu amwite nyau paka kibichwa natamani nitoke nimjibu...namsikia mume wangu anasema)

" Mama samahani mke wangu kuna kitu amekukosea au?

" Amekukosea wewe kama alikuwa anakupenda angezaa uko nyau wake.

" Tambua mama mke wangu akunificha kitu wakati naenda kumuoa ata wewe sikukuficha uliniambia oa tena uyo ndio mwanamke aliyekomaa akili anayelea mtoto peke yake Leo unamtukana halima mama una nini?

" Nenda kapumzike kesho asubuhi nataka kukwambia kitu tena ukifate.

" Sawa.

( Mume wangu aliingia chumbani akanikuta nalia...akanibembeleza nikanyamaza akaenda kuchukua chakula akanilisha mimi uku sina amani nikamwamsha mwanangu nikamlisha...siku ikapita asubuhi asubuhi mama mkwe kaja kugonga mlango na mume wangu akatoka yeye akaanza kusema)

" Unaona umeoa mke asiye jielewa amesikia sauti yangu ndio imesema hodi anakuacha wewe uje ufungue mlango je ningekuwa sina nguo?.

" Mama Jana uliniambia asubuhi unataka kuniambia kitu ndio maana nimewai mimi kufungua kwa hili mbona mke wangu kosa ana.

" Sasa sitaki maneno mengi mimi ndio mama yako nimekuja na swala moja tu nataka uoe mke wa pili.

" Mama nioe mke wa pili?

" Ndio tena mke nakuchagulia mimi uyu si umemchagua wewe mwenye kinyau nataka uoe mwanamke mnafanana wote amna mtoto.

" Mama usiite nyau kwenye maongezi yetu.

" Koma wewe uwezi kunizuia mimi kumwita halima nyau sasa upo tayari kuoa mke wa pili?

" Sipo tayari. 

" Nipe vigezo ambavyo aupo tayari. 

( Mala namsikia baba mkwe anaongea)

" Juma acha nimpe kigezo mimi mke wangu juma ayupo tayari kuoa mke wa pili mpaka baba yake nioe mke wa pili je mke wangu upo tayari nikaoe mke wa pili?

" Unasemaje wewe?

" Upo tayari nikaoe mke wa pili?

" Baba juma mimi naongea na mwanangu sitaki kuniingilia. 

" Na mimi naongea na wewe nyau wetu atulie.

" Nyau nani?

" Juma.

" Mume wangu umeanza kurukwa na akili au?

" Ninazo sana nyau Ingia ndani niache nionge na mama yako.

( Mume wangu anaingia ndani mama yake anamzuia anasema)

" Wewe sio nyau...ni mwanangu achana na baba yako nisikilize mimi upo tayari kuoa mke wa pili?

" Mama jibu Basi swali la baba je na wewe upo tayari baba akaoe mke wa pili?

( Mama mtu kilimtoka kibao kimoja cha nguvu kampiga mume wangu)

"Paaaaaaaa"

" Koma usije kurudia tena kuniambia ilo neno sasa nakwambia kwa msisitizo utaoa uoi mke wa pili...

ITAENDELEA 
KARIBU KWENYE SIMULIZI MPYA GUSA ACHIA TWENDE CHUMBANI BABA MKWE...SIMULIZI IPO FULL VISANGA KAMA VYOTE JE NINI KILIENDELEA USIKOSE EPISODE IJAYO....*

GUSA ACHIA TWENDE  CHUMBANI BABA MKWE
Sehemu ya pili.
👉 Koma usije kurudia tena kuniambia ilo neno sasa nakwambia kwa msisitizo utaoa uoi mke wa pili..👇

( Mume wangu akujibu aliingia ndani moja kwa moja kuugulia maumivu yake ya kupigwa kibao...mimi nilikuwa nimejifunika shuka kama sijui kinachoendelea na mume wangu akutaka kuniamsha akawa amekaa kitandani amejiinamia tu...mimi nikaamka nikamsalimia nikaenda kufagia uwanja kama sijui nini kinaendelea)

" Wewe mama nyau.

" Mama mama nipo chini ya miguu yako naomba usiniite ilo JINA.

" Mimi naondoka zangu kazini akiamka uyo mumeo mwambie mama  kasema utaoa mke wa pili utake usitake aya acha kufagia kwanza kamuweke maji baba yako akaoge.

( Niliona kabisa hii sio heshima mimi ndio nikaweke maji ya kuoga ya baba mkwe...sikutaka kupinga nikaenda kumuwekea natoka chooni ananiambia)

" Aya nyosha shati lake hili pasi akikisha baba yako katoka wewe ndio ufanye kazi zengine sawa.

" Sawa mama.

( Yeye akaondoka mimi nikafanya alivyoniagiza...na baadae  baba mkwe na yeye akaondoka...mume wangu alipoamka Nikamwambia alichosema mama yake ila akunijibu akaondoka...nikabaki mimi na mwanangu yani halima ajui chochote yeye ndio kwanza ananiambia)

" Mama lini nitaanza shule?

" Mwakani mwanangu utaenda shule sawa.

" Sawa mama.

" Aya kula upumzike.

" Sitaki nataka tucheze mapera uko.

( Napenda kumfurahisha mwanangu Basi nikawa nacheza nae mapera yeye anaimba)

🎼 Mapera mapera baba kaleta ugali na kifaranga cha kuku we tia apa tia apa...shishishi.

( Yani full furaha ajui changamoto iliyo mbele yangu..upande wa mume wangu akaenda kwa rafiki yake anaitwa hasani kuomba ushauri juu ya mama yake akamwelezea mwanzo mwisho hasani akamwambia)

" Juma ungeenda kupanga aya yote yasingekuwepo ila ukikaa na wazazi alafu wewe upo peke yako mkeo atapata tabu sana.

" Hasani napenda nitoke nyumbani ila mama alishaniambia Siku nitakapotengana na yeye yani nitoke pale nyumbani Basi ndio mwisho wa maisha yake anataka niishi na yeye pale.

" Sasa kama kuishi na wewe akuache uwe huru na unayoyafanya unadhani pale mkeo si atakuwa kama mfanyakazi wa mule ndani ila kama utakuwa huru utatafuta mfanyakazi hili mkeo akae kama mke na si mfanyakazi ila ukienda kuoa mke wa pili ambaye anayempenda mama yako watashirikiana kumtesa mkeo yule mama halima.

" Hilo naliwaza sana nafanyaje sasa maana naogopa ladhi vile vile.

" Kaonge na mzee wako atakupa njia.

( Mume wangu akampigia simu baba yake na baba yake akupokea simu...alikuwa bize na kazi...basi jioni ikaingia wa kwanza kuludi baba mkwe akaingia zake ndani...mimi nikaanda chakula cha usiku mala mama mkwe na yeye analudi tena kaja na mwanamke amejazia kweli kweli ananiambia mimi)

" Wewe mama nyau mumeo karudi?

( Ilibidi nijibu tu)

" Ajarudi.

( Halima mwanangu akaniliza akaniuliza)

" Mama wewe ndio mama nyau?

" Ndio mwanangu.

" Nyau mwenyewe yupo wapi?

" 😭😭😭😭.

( Mama mkwe akasema)

" Wewe acha kuchura apa mpoke pochi mke mwenzio uyo uyo ndio ataolewa na mwanangu toto toto ajazaa wala ajawai kushika mimba vyote anakuja kuvipata kwa mwanangu aya mpokee pochi ilo.

( Yule mwanamke akalitoa pochi kwenye bega kalishika mkononi ananipa kwa dharau yani nikampokee tena anasema)

" Apokee uku amepiga magoti kwetu ndio heshima njoo uchukue pochi mke mwenza..

ITAENDELEA..
Je itakuwaje...?

GUSA ACHIA TWENDE  CHUMBANI BABA MKWE
Sehemu ya tatu. 
👉 Apokee uku amepiga magoti kwetu ndio heshima njoo uchukue pochi mke mwenza....👇

( Kwakweli niliumia sana moyoni nasema ni Bora ndoa ife ila zarau izi apana kabla sijamjibu namsikia baba mkwe anafoka tena anakuja tulipo)

" Wewe mwanamke ni mke wa nani mpaka utake kumsumbua mama halima hii nyumba  ni yangu na uwezi kupanga ujinga wako humu ilo pochi lako kaa nalo kama unavyokaa nalo pochi lengine ilo kama wewe unataka kupokelewa pochi lete kwanza pochi manyoya kwangu nilipokee. 

" Mume wangu unatukana ivi una nini?

" Uyu anavyotukana unaisi ana nini ananing'iniza kikono apa nipokee uku umepiga magoti aya alilete pochi manyoya kwangu nampokea uku nimesimama.

( Duu nikasema kimoyoni kumbe baba mkwe ndimu ila alitulia tu na ndio mtetezi wangu...yule msichana alikaa kwenye sofa kimya mbwembwe kwisha...mimi nikanyanyuka na halima wangu uyo naenda zangu chumbani kumbe chozi linanidondoka mwanangu analifuta ananiambia)

" Mama usilie ukilia unaniliza mimi.

( Kha nikashangaa mwanangu anasikia uchungu mimi nikilia...nikamwambia)

" Sirii tena aya tufanyaje ulale.

" Tucheze ukuti mama.

( Mwanangu anapenda michezo Basi nilicheza nae ukuti ndani nimpe furaha...maumivu nibaki nayo mwenyewe kweli alisikia raha akalala...mala mume wangu anakuja namsikia sebuleni uko)

" Shikamoo mama.

" Marhaba mwanangu dume la mbegu lililokosa shamba la kuweka mbegu zake sasa nimekuletea shamba safi alijawai kulimwa hili mwanangu aya kaa chini apo.

" Ngoja nikamsalimie kwanza mke wangu. 

" Yupo ametoka sasa ivi na mwanawe kaa kwanza apa mwanangu wewe.

" Sawa aya niambie.

" Mwanangu uyu ndio yule mke niliyekwambia utaoa.

" Mama ata kama dini imeruhusu ila mimi natakiwa nishauriane na mke wangu. 

" Wewe usitake niseme neno sio saizi yako ushauriane na mkeo ndio anayelala nae.

" Mama mimi kwenye maisha yangu sikupanga nioe matara.

" Dini inasema wake wanne ongeza mke uyu.

" Ngoja Basi nionge ata na baba.

" Yupo ndani humo Leo kaamka na matusi uonge nae nini kwanza uoni mtoto mtoto kweli nyanyuka kwanza akuone mbona umekaa mume ndio uyu mtoto ana nyashi sio yule ana makanyagio.

( Mama mkwe ananiponda mimi..kweli uyo mwanamke akanyanyuka akamwambia mume wangu)

" Nakupenda mume wangu mtalajiwa nilikuwa na ndoto ya kuolewa na mwanaume ambae mama yake ndio kanitafuta naona ndoto yangu imetimia.

" Juma usikae kama zuzu nimekitunza kitovu chako mimi vizuri uje uwe vizuri kweli kweli aya mpe mkono mwenzio alafu uingie ndani uko kwa kinyago cha kimakonde.

( Mume wangu alipo mpa mkono tu yule mwanamke apo apo akasema)

" Mama naoa mke wa pili.

( Nililia mimi ndani peke yangu kauli ya mume wangu iliniliza sana natamani baba mkwe atokee avuruge maongezi ila naona kimya sijui baba mkwe kalala...mama mzazi wa mume wangu anasema maneno ambayo apaswi kusema mzazi anamwambia mume wangu)

" Aya nenda nae kalale nae hotelini uko mwanangu vipi unataka kuoa kizamani uuziwe mbuzi kwenye gunia ata karanga za kapu unaonja kwanza.

" Sawa mama.

( Nilitamani nitoke nguvu sina najikuta napiga magoti NALIA tu...mume wangu akuingia ndani ameishia sebuleni ameondoka na yule mwanamke ameenda kuonja ladha yani mume wangu ameenda kuzini...nimelia usiku kucha...asubuhi naamka nakutana na rundo la nguo nifue tena mama mkwe anasema)

" Ufue haraka izi upange vizuri apa ndani kuna wazee watakuja nataka niwatume barua wapeleke nyumbani kwa mke mwenzio sawa.

( Niliitika kwa kichwa...mama mkwe akaondoka...mala anaamka baba mkwe ananiambia)

" Acha kufua na usilie ngoja nimwite Dobi. 

( Nilimwambia)

" Akija akimuona dobi itakuwaje. 

" Yule arudi sasa ivi wewe nenda kalale upumzike.

( Kweli nilienda kulala kidogo nikachukua simu nampigia mama yangu mzazi namwambia yaliyojili ananiambia)

" Sasa wewe unaogopa matara mbona mama yako nilikaa kwenye matara tulia kwa mumeo iyo sio sababu ya wewe kuwa mnyonge.

" Mama ndoa yenyewe mama mkwe ndio kailazimisha. 

" Mumeo kataka wewe sisi wanawake ndio tunaolewagwa ata na tusio wapenda muda mwengine kutoa mkosi ila sio wanaume.

" Mama mimi naomba taraka. 

" Koma tena ukome kama ulivyokoma kunyonya ziwa langu uombe taraka pambana kwenye ndoa yako.

( Nilikata simu nikaanza Kulia tena mama yangu mzazi ananiambia nikome yani nipambane kwenye ndoa yangu yani mama yangu amekata kukaa na mwanangu aliniambia awezi kunilea alafu aje anilele mwanangu mimi sikulelewa na bibi yangu nikomae na mwanangu Leo ananiambia nipambane na ndoa yangu...baba mkwe kweli alimleta dobi alifua fasta akamaliza na alifanya usafi ndani akamaliza akaondoka kabla ata mama mkwe ajaja...akaja kunigongea mlango akaniambia)

" Mimi natoka nadhani kila kitu kipo sawa.

" Asante baba.

" Usilie nipo kwa ajiri yako.

( Neno yupo kwa ajiri yangu lilinistua yupo iyo kivipi ila nikasema)

" Sawa silii baba.

" Aya shika pesa hii baadae kamnunulie halima nguo ila ukitaka kuondoka umuage mumeo. 

" Sawa.

( Aliondoka nikaangalia pesa zile naona laki na nusu nikawa nawaza kuondoka tu kwenye ndoa hii ndio nauli ila nawaza naenda wapi?...nikachukua simu nampigia mume wangu nimuage naenda kununua nguo za mtoto simu inaita anapokea mwanamke yule)

" Haloo.

" Samahani naomba umpe simu mwenye simu yake.

" Anaoga ulikuwa unasemaje?

" Akirudi kuoga anipigie. 

" Mmm akirudi kuoga anaendelea na starehe maana tamu si mchezo aichoshi wewe sema tu ulikuwa unasemaje.

( Nilikata simu...machozi yananitoka...halima anaamka ananiita)

" Mama mama mama.

" Bee mwanangu. 

" Unalia tena?..mama kwani siku izi una nini unalia lia ovyo.

( Nilitamani nijikaze chozi lisinitoke nisimpe majonzi mwanangu ila ikawa ngumu chozi linadondoka...na mama mkwe anaingia akiwa na wazee wawili uku wameshika barua na bahasha mixsa leso yani mpango wa kuchumbiwa mke wa pili wa mume wangu unafanyika sebuleni mama mkwe ananiita ananiambia)

" Aya watengeneze juice washenga awa wa mke mwenzio matunda yapo apo kwenye friji changamka hili ipate baridi fasta wanywe waende.

( Duu nipo kwenye mtihani mzito nitengeneze juice ya washenga mimi 😭)

ITAENDELEA*

GUSA ACHIA TWENDE  CHUMBANI BABA MKWE
Sehemu ya nne.
👉 Duu nipo kwenye mtihani mzito nitengeneze juice ya washenga mimi😭...👇

Bahati nzuri wazee wale mmoja apo akasema)

" Mama usipate tabu swala la kuandika barua alichukui Muda mlefu muache binti atulie tu.

" Sawa wazee wangu andikeni basi.

( Mimi nikasema kimoyoni wazee wameona mbali wanajua kabisa mimi sifurahi kinachofanyika alafu nitengeneze juice naweza kuwawekea chumvi kwenye juice...niliingia ndani naona mama alinipigia simu mala mbili nikampigia akaniambia)

" Kuna ujumbe nimekutumia apo kwenye simu yako usome ujitambue.

" Sawa.

( Nilienda upande wa sms naona ujumbe mlefu unasema)


" Mwanangu Epuka matapeli , Dunia nzima hakuna mwanaume anayekupenda kuliko mume wako,

Hata waje na swagah na maneno mengi ya ushawishi mume wako ndiye aliyekupenda ,, waache na magari yao na pesa zao , hata kama wanamzidi mumeo Kila kitu , still Baki na mumeo..

Mume aliyekuoa amekufanya

1. Uheshimike 
2. Uaminike 
3. Uthaminike 

Acha ujinga na ulimbukeni yaani mtu unavutwa na vitu usivyojua vimetoka wapi ,,unaanza  kuonyesha dharau kwa mumeo kisa mwanaume wa mtaani  kakupandisha kwenye gari basi unadharau mumeo,!!! 

Kuna wanawake hawajielewi anakutana na mwanaume anampa hela ya wigi basi anasahau mume ambaye anamhudumia siku zote za maisha yake kisa wigi na chips ..yaani wigi linafanya asahau mengi mazuri ya mumewe,

Wewe upo kwenye ndoa heshimu mumeo, tulia naye ,,achana na tamaa komaa na mumeo ipo siku mtainuliwa tu ,,  mume ni mume tu thamani ya mume kamwe hailingani ya tapeli wa barabarani hata kama ana ndinga Kali ..

Mume thamani yake haipimwi kwa vitu Bali namna alovyojitosa kati ya wengi kukuoa huyo ni mtu na nusu , wengine kazi yao ni kuchezea tu visima lakini si waoaji ...

Usimdharau mume kisa Hana gari 

Mheshimu sana..mwaume aliyejitoa kukuoa 

Kama huamini hangaika tu siku akikuponyoka ndo utakuja kujua ulikuwa hujui"

( Nikajiuliza uyu mama akunielewa au?...mimi sina bwana wala simdharau mume wangu ila mume anataka kuoa mke wa pili yeye SMS ndefu kwangu aina mashiko yoyote nikazima simu...mala nasikia wazee wanaaga)

" Sisi tunaenda.

" Sasa wakisema mahari mnipigie nitume hapo hapo na mpange TAREHE ya ndoa Leo Leo mambo yaende fasta aya.

" Sawa.

( Wazee wakaenda...mama mkwe ananiita mimi nikatoka akaniambia)

" Mpikie mtoto chakula ale alafu uje unifanyie kazi yangu moja.

( Leo sikuumia kamwita mwnanangu mtoto Bora amwite mtoto kuliko kumwita mwanangu nyau...nilimpikia chakula mwanangu akawa anakula sasa mama mkwe ananiambia)

" Kachukue chanuo unifumue nywere izi unikwangue m-ba...nataka nikasuke msuko huo siku ya harusi wajue mimi nani.

( Moyoni naumia ila nikaona nimfumue tu nywere kweli nilimfumua  nikamkwangua kichwani uku akili zangu zinasema ingekuwa akuna polisi namkandamiza na chanuo la utosini uyu....uku naendelea kukwangua nikamaliza kukwangua akaenda kuosha nywere saloon..baba mkwe na yeye akaja kabeba mfuko nikampokea akaniambia)

" Mfuko wako huo.

" Asante. 

( Nikaingia nao ndani naona nguo za mwanangu nzuri sana nikasema baba mkwe anampenda mwanangu akaniita akaniambia)

" Mama halima kesho saa 12 nipigie simu kuna kitu nataka nionge na wewe ila ukiwa unanipigia akikisha akuna mama yako wala mumeo sawa.

" Samahani si uniambie sasa ivi apa akuna mume wangu wala mama mkwe.

" Kesho sio Leo wewe liweke kichwani ilo.

" Sawa.

( Mala nasikia hodi naenda kufungua ni mume wangu na yule binti wamevaa tshirt sale la mume wangu limeandikwa (Lo) la yule binti limeandikwa (ve) nikiunganisha napata neno love....niliumia sana mume wangu ananiambia)

" Chakula tayari nasikia njaa sana.

( Kabla sijamjibu yule mwanamke anasema)

" Ivi uyu kashawai kukupa mpaka ukasikia njaa?

( Dah swali kaulizwa mume wangu ila mimi kanitusi nishaelewa alichomaanisha natamani nimjibu ila nasema nitaleta ugomvi yani yule mwanamke akambusu mume wangu mbele yangu)

" Mmmwaaaaaaa...

ITAENDELEA

GUSA ACHIA TWENDE  CHUMBANI BABA MKWE
Sehemu ya tano.
👉 Mmmwaaaaaaa...👇

( Baba mkwe akamfukuza yule mwanamke kwa kalipio Kari sana)

" Wewe mshenzi wa tabia ujaolewa unaanza zarau yani unampiga busu mwenzio mbele ya mkewe ujafundwa kwenu wewe aya ondoka  sasa ivi kabla sijakutandika dangaladeshi wewe.

( Cha ajabu mume wangu akaondoka na yule binti...akili yangu nikasema nayo mume wangu itakuwa karogwa sio akili yake ivi inawezekana kweli akubari nidhalauliwe ivi...njiani uko wanakutana na mama mkwe na mama mkwe akaambiwa yaliyojili uku akawaambia)

" Sasa binti usiwe na wasiwasi wewe nenda nyumbani kwenu ukajiandae na ndoa mahari nishatuma na tarehe ya ndoa wiki ijayo na wewe kuanzia sasa ivi utaenda kulala hotelini mpaka siku ya ndoa sawa.

" Sawa mama.

" Aya twende Ukaone hoteli niliyokuchukulia.

" Sawa mama.

( Wakaondoka mpaka kwenye hotel ambayo mama mkwe amekodi hili mume wangu asirudi nyumbani...uku mimi nampigia simu mama namwambia yaliyojili na mama ananiambia)

" Wewe mama halima kikuumacho wivu tulia mumeo aoe apange siku za kulala kwako na kwa mwenzio.

" Ila mama sasa ivi maladhi mengi sana ivi kwanini nisiombe taraka tu.

" Nimekwambia sitaki kusikia ilo neno.

( Nilikata simu nawaza sana juu ya maisha yangu...nilitoka kwenda sokoni nipo na mwanangu naongea peke yangu juu ya maisha yangu nikawa nawaza tena baba mkwe anataka kuniambia nini na kwanini aniambie kwenye simu sio macho kwa macho...nilifika sokoni nikaona watu wengi wamesimama sehemu na mimi nikaenda ndio namuona jogoo poll anaongea)

" Hakuna mwanaume wa kweli anayetaka mke asiyekuwa na busara. Ni wavulana wasio na nia thabiti wanaopendelea wapenzi wa aina hiyo. Usikubali kudanganywa na mvulana anayekutaka kwa ajili ya anasa kila mwishoni mwa wiki, anayekushawishi uvae nguo za kubana, utumie vipodozi vya kufurahisha macho ya watu, na kunywa pombe kupita kiasi. Mwanamume wa namna hiyo hana mpango wa kukuoa.

Mvulana anayependa kuzungumza maneno machafu na kutaka ngono kabla ya ndoa anakuchukulia kama chombo cha starehe. Hilo ni onyo la mapema kuwa hatakuheshimu baada ya ndoa.

Je, umewahi kujiuliza kwa nini wanaume wengi wanatafuta wake wenye tabia ya utulivu badala ya kuangalia urembo wa nje? Hii ni kwa sababu wanaume wanahitaji wake wenye moyo safi na wenye maadili ya kweli. Mwonekano wa nje unaweza kupungua, lakini utu na hekima ya ndani hudumu. Wekeza zaidi kwenye tabia yako na utu wako.

Mwanaume wa kweli anatamani nyumbani palipojaa utulivu na mwanamke mwenye akili timamu, anayeweza kulea watoto wake, kushirikiana naye katika maamuzi makubwa, na kuwa nguzo ya faraja kwa familia. Mwanamke wa aina hiyo ndiye anayeheshimiwa kama mama, dada, na mke wa kweli.

Hii haimaanishi kuwa urembo ni vibaya; ni vyema kuonekana vizuri. Hata hivyo, usisahau kuwa maadili na hofu ya Mungu ni muhimu zaidi. Biblia inasema: "Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; bali mwanamke amchaye Bwana ndiye atakayesifiwa” (Mithali 31:30).

Je, unamtanguliza Mungu katika maisha yako? Mwanamume anayemcha Mungu atavutiwa na mwanamke mwenye adabu, mwenye hofu ya Mungu, na mwenye maadili. Usiruhusu mwanaume yeyote akutumie kama chombo cha kupita wakati.

Hivyo hivyo, usikubali kuwa na mwanaume asiye na hofu ya Mungu, haijalishi ana mali au pesa kiasi gani. Heshimu maisha yako, jitambue, na mche Mungu kwa kila jambo.

( Nilipata mwanga kichwani mwangu mimi nipo na mwanaume asiye mche Mungu nilienda mbele kuomba kuongea na jogoo poll kweli niliweza kuongea nae na kumuomba ushauri juu ya maisha yangu akaniambia)

" Nakushauri mwambie mumeo akapime kabla ya ndoa hili uwe na amani anapokuwa amepanga siku zile tatu uku tatu kule siwezi kukwambia uombe taraka wakati ndoa za matara zipo kwenye imani ya kiislamu japo mumeo akupita kwenye njia sahihi ila..

" Nimalizie tu jogoo nakuomba. 

" Siku nyengine acha niwai zangu istoriya yako imeniumiza kidogo na imenifunza kitu kuna wanawake wengine wana roho izo kumbe duniani kuna mengi. 

" Lini nikutafute jogoo 

" Chukua namba yangu ya simu hii 06556..... utanicheki acha niende.

" Sawa.

( Nililudi nyumbani nawaza nitamwambiaje mume wangu jambo la kupima?...niliwaza nikawazua siku ikaisha kesho yake nimeshinda nawaza tu ikafika Muda ambao baba mkwe aliniambia nimpigie simu saa 12...na alikuwa ayupo mtu yoyote nyumbani nikampigia simu akapokea alinistua alipoanza kuniambia)

" Mama halima unaweza kukaa na siri?

" Siri gani baba niambie. 

" Nijibu kwanza unaweza kukaa na siri nataka kukusaidia sehemu kubwa ya maisha yako.

" Ndio uniambie sasa baba Siri gani.

" Mama halima mimi na.......?

ITAENDELEA 
Mwisho wa kionjo..
Nini KILIENDELEA NUNUA simulizi usome kwenye simu yako.. Kwa shilingi 2500 Tu
kslprojects

kslprojectstz@gmail.com Entrepreneurship Power

Post a Comment

Previous Post Next Post